Alhamisi, 13 Julai 2017

Prof. Mdoe afanya mazungumzo na uongozi wa Uranium One


Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe amekutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa kampuni ya Uranium One na Mantra Tanzania ambao wanamiliki leseni ya uchimbaji wa Madini ya Urani kwenye eneo la Mto Mkuju Kusini mwa Tanzania. Mantra ni sehemu  ya  kampuni ya Uranium One na kampuni ya kimataifa ya madini ya ROSATOM-ya Shirikisho la Serikali ya Urusi ya Nishati ya Nyuklia.

Kaimu Katibu Mkuu,Wizara ya Nishati na Madini,  Profesa James Mdoe akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Uranium One, Vladimir Hlavinka katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. Katikati ni Rais wa Uranium One Group, Vasility Konstantinov.


Kikao hicho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano kati ya Tanzania na kampuni hizo, kuporomoka kwa bei ya Urani katika soko la dunia na kampuni hizo kushirikiana na STAMICO katika miradi ya uzalishaji madini.

Rais wa Uranium One Group, Vasility Konstantinov aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano inaoendelea kuutoa kwa kampuni hizo ili kuhakikisha kuwa lengo la kampuni hiyo kuendeleza mradi wa uchimbaji madini ya urani nchini linafanyika kwa ufanisi.

Konstantinov pia alitumia nafasi hiyo kukanusha habari zilizoandikwa katika baadhi ya magazeti nchini hivi karibuni kuwa kampuni ya MANTRA Tanzania imesitisha (Suspension) uchimbaji wa Madini ya Urani kwenye leseni yao iliyoko eneo la Mto Mkuju moja ya sababu ikiwa ni mabadiliko katika Sheria ya Madini.

Soma maelezo mengine hapa:
https://issamichuzi.blogspot.com/2017/07/prof-mdoe-afanya-mazungumzo-na-uongozi.html

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni