Alhamisi, 13 Julai 2017

Dar es salaam ni miongoni mwa majiji 10 masafi Afrika

Africa inaeldelea kukua kwa kasi, huku jiji la Dar es salaam likiwa ni moja mwa majiji  masafi barani Afrika. Japo kuwa miaka kidogo ya nyuma ilionekana kuwa jiji la Dar es salaam ni miongoni mwa majiji machafu duniani. Kwa sasa Dar es salaam imetajwa kuwa ni miongoni mwa majiji kumi masafi barani Afrika.
Jiji la dar es salaam


Hii ni kutokana na juhundi mbalimbali za wananchi wakishirikiana na serikali, ndio maana sasa nasi tumeanza kuonekana kimataifa. Hatutakiwi kubweteka sasa ni muda wa kujitahidi zaidi ili hapo baadae tuwe ni miongoni mwa majiji masafi duniani.

Zile tabia za kutpa tupa taka ovyo, tuache. Huku viongozi wa serikali za mitaa wakishiriki kikamilifu katika kuhamasisha usafi. Unajua tunapokuwa tunafanya usafi vizuri na jiji letu la Dar es salaam likawa safi, tutaweza kuvutia wawekezaji, watalii na isitoshe tutakuwa na afya njema.

Mtandao wa African Zeal umetaja na kueleza kuwa kati ya majiji 10 barani Afrika Dar es salaam imechukua nambari tisa. Ni kama hapo chini:

CityCountry
1. Cape TownSouth Africa
2. Port LouisMauritius
3. JohannesburgSouth Africa
4. NairobiKenya
5. GaboroneBotswana
6. TunisTunisia
7. AccraGhana
8. LibrevilleGabon
9. Dar es SalaamTanzania
10. WindhoekNamibia

Unaweza ukasoma zaidi hapa ili upate maelezo zaidi:
http://www.africanzeal.com/cleanest-cities-in-africa/

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni